MAONYESHO YA NANE NANE- barmedas.tv

MAONYESHO YA NANE NANE 2014 YAFUNGULIWA.

Maonyesho ya wakulima ambayo hufanyika Kila Mwaka mwezi wa 8 Nchini kote, hapa katika Mkoa wa Mwanza maonyesho haya yamefanyika maeneo ya Nyamhongolo- nje kidogo ya Jiji la Mwanza.

Eneo hili la Nyamhongolo ni eneo lilitengwa raimi kwa ajili ya maonyesho ya kiubiashara , maonyesho haya yamefunguliwa tarehe 5 August  2014 na Mgeni rasimi kutoka Geita Mh: Magalula Saidi Magalula.

Kabla ya mgeni  Rasmi  kuanza kuhutubia, alitanguliwa na mwenyeji wamke Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng  Evarest  Ndikilo ,ambaye alieleza mafanikio  ya maonyesho ya Nane Nane Mwaka huu 2014  yamefana sana kjwani Mwaka jana 2013 ni Makampuni 50  tu yaliyoshiriki maonyesho hayo,tofauti kubwa na Mwaka huu ambapo Makampuni 230 yamejitokeza na kushiriki maonyesho haya hii inaonyesha Halimashauri 31 kati ya 41 zimeshiriki maonyesho haya.

Akieleza mafanikio ya ushiriki wa Makampuni hayo yaliyojitokeza kwa wingi kiuonyesha shughuli kubwa, aliendelea kumufahamisha mgeni wa Maonyesho hayo  ambaye pia ndiye alifafanua  maonyesho hayo kwa kusema, Mwaka kesho  Mkoa umejipanga kufanya maandalizi makubwa nakuhakikisha maonyesho  2015 yatakuwa ni makubwa na  yakuvutia,   na hatua nyingine ni  kujenga majengo ya kudumu katika maeneo hayo.

Maeneo yataendelea  hapo takribani  wiki nzima hivyo, watu watapata nafasi yakwenda kutazama na kujipatia  kwa kununua bidhaa za Kitanzania ikiwa  ni mazao ( Product )  za Kanda ya ziwa.

KARIBUNI KWENYE MAONYESHO YA WAKULIMA - NANE NANE  2014.

Picha chini zinaonyesha shughuli nzima za ufunguzi wa maonyesho hayo.



Comments

Popular Posts