TAMASHA BUJORA-barmedas.tv

Tamasha la Ngoma na Utamaduni wa msukuma linaendelea kupamba moto katika uwanja wa michezo Kisesa,   Tamasha hili limeandaliwa na kituo cha Makumbusho Bujora kwa kushirikiana na kituo cha utangazaji barmedas.tv wao wakiratibu shughuli zote zinazofanyika hapo tangia mwanzo wa Maonyesho hadi mwisho ambapo itakuwa siku ya Jumatatu ndipo hitimisho ya  Tamasha hilo.

Tamasha hili limekuwa kivutio kikubwa na majira ya kuanzia saa 10:00 jioni Watu wanaanza kufurika kuja kujionea utajiri wa ngoma ulioko huku Kanda ya ziwa haswa ukiongozwa na kabila hili la Kisukuma inaonekana kabila hili lingali likienzi utamaduni wake, akiongea mkiuu  wa kituo cha Makumbusho ya Bujiora Fr  Shija alisema kweli siku za nyuma sherhe hizi za Bulabo zilikuwa zimeanza kudorora lakini Mwaka huu kumekuwa na mwamko mkubwa sana na Mwaka kesho anakisia kutakuwa na mwamko mkubwa sana.


Comments