MISS LAKE ZONE-barmeda.tv

MISS LAKE ZONE:

Jana tarehe 29/08/2014 kuanzia saa 5:30 Asubuhi, tulitembelewa na ugeni katika ofisi zetu za



barmedas zilizoko Mtaa wa Bantu, bada ya maelezo na kutembelea shughuli zote Picha  nyingi zilipigwa kwa ajili ya kumbu kumbu, kama zinavyonekana hapo juu.

Ugeni huo ulikuwa umejaa furaha baada ya kumaliza kiu ambayo walikuwa nayo kuwa haitakuwa vyema kuondoka katika jiji hili pasipo kufika katika ofisi hizi za barmedas angalau kuweka hata baraka zao, kweli ilipofika majira hayo, mwandaaji wa shiondano hili Flora Salon alinipigia simu Uncle Sokoro tumo njiani tunakuja! nami niliitikia karibu sana.

Kweli ugeni ulitinga na kusalimiana kulingana na jinsi mtu alivyoona itamfaa maana kulikuwa na umri mbali mbali kwa wageni hao na wenyeji wao. walikaribishwa nakuingia ndani na jambo lakwanza ilikuwa kutambulishwa shughuli zote zinazofanywa na barmedas.tv haswa kwa kueleza  channel zetu tulizonazo na huduma zetu kwa wateja.

Kilichofuata nikutambulishana wenyeji pia wageni, zoezi lilipomalizika , kikafuata kipindi cha wageni kuuliza  maswali kutokana na maelezo   ambayo yalichukua takribani  nusu saa ,  maswali makuu   yalilikuwa Je Huduma zenu barmedas zinawafikia wateja kama walivyo kusudia?
2. Nini faida ya Tv zile kubwa za Barabarani  je watu wanajali kuziangalia? kwa kuwa ziko maeneo ya purukushani sana akazidi  kwenda kwa undani zaidi  "mimi nahisi watazamaji ni wachache labda"
3.Je pia munajishughulisha na jamii ni kweli ?  maana tumepata sifa zenu kuwa barmedas mko mbele sana kwa shughuli za kijamii na ndio pia  wito wetu mkubwa kuja kwenu maana sisi Miss Lake zone tunamalengo hayo"
Namaswali mengine mengi, kwa ujumla maswali yalijibiwa kwa ufasaha na mwisho Miss Lake Zone walipiga makofi kuashilia kuwa kila kitu walichoiliza kimejibiwa kwa ufasaha mkubwa.

Comments