SEMINA YA MAWAKASEGE-barmedas.tv

Semina ya Mwalimu Christopher Mwakasege yamalizika jana tarehe 25/08/2014 katika viwanja vya Furahisha  Jijini Mwanza.

Kila Mwaka  Semina ya Mwalimu Mwakasege hufanyika katikla viwanja hivi na majira kama haya, semina hii hukusanya watu mbali mbali ambao huja kumsikiliza Mwalimu Mwakasege akitoa mafundisho ya neno la Mungu.

Mwaka huu Kituo cha barmedas.tv hakikurusha semina  ya Mwalimu Christopher hii nikutokana na kituo hiki kuwa katika mabadiliko ya mfumo wa  Digital hivyo  iko katka kubadiliko   vifaa mbali mbali na pia uboreshaji wa mitambo yake kufikia kiwango cha HD .

Mkurugenzi wa Barmedas.Com Bwana Hirnoy Barmeda, akiongea na baadhi ya watazamaji waliokuwa wamezoea kupata semina ya Mtumishi wa Mungu Mwalimu Christopher Mwakasege kuangalia moja kwa moja kupitia Channel zake  je Mwaka kesho itakuwaje? alijibu,  kwa kuwahakikishia watazamaji na wapenzi wa semina ya Mwalimu Mwakasege kuwa 2015 kutakuwa mambo mengi yameboreshwa hivyo watazamaji wategemee semina ya Mwakasege kuonekana kwa kiwango cha hali ya juu na pia masafa yataongezeka.

Picha zinaonyesha Wahudhuliaji wakirudi nyumbani kwa kutafuta usafiri kwa wakazi  wanaoishi kwenye vitongoji kama , Igoma ,Nyakato, Mabatini ,Buhongwa, Kisesa, Sengerema ,  Magu , Kayenze na sehemu zingine nyingi ambazo zinahitaji usafiri kurudi nyumbani.

Comments