MITAA YA MWANZA-barmedas.tv

Baadhi ya mitaa katika Jiji la Mwanza, kila mji hata mikubwa ulimwenguni huwa kuna majumba ambayo hubaki ni kumbu kmbu na alama katika mji huo kwa ajili ya kumbu kumbu.

Mitaa iliyoko katikati ya Jiji la Mwanza hukumbusha na huleta taswira ya kuonyesha hakika mji  ulianza vipi na hadi hapo ulipofikia, lakini pia kuna waanzilishi wazee ambao walisifika kipindi kile ambapo sasa huenda wametoweka katika ulimwengu huu  lakini wangali wanakumbukwa kutokana na alama mbali mbali ambazo zingali zipo zikionyesha uhalisia.

Zipo alama nyingi ambazo ukiziona zinakurejesha huko nyuma haswa kwa watoto waliozaliwa hapa baadae kwa njia moja ama nyingine wakawa wameondoka katika Jiji hili kwa ajili  ya kujitafutia  riziki wanapoona majengo kama haya yana kurejesha kabisa nyuma huenda na kukufanya machozi yakulenge lenge kwa kukumbuka mbali sana.

Baadhi ya mitaa ambayo ilisifika sana huko nyuma ni kama , Seleman Nassoro, Mtaa wa Nera, Mlima wa Machemba, Kirumba, Kigoto, Mabatini, Mkenyuke, Kigoto, Igogo, Mwaloni Kirumba, Kwa Pagonisi nk

Watu wa zamani maarufu ambao ni alama ya Mwanza,ni kama , Shekh  Amini- Rufiji, Mzee Hussein Shelali- Rwagasore, Mzee Mabruki - Karuta na Band ya Johari Taarabu  ,   Mzee Liami- Kenyatta Road, Mzee  Juma Kafiti, Mzee Kahungwa, Mzee Busigasorwe, Mzee Magongo, Gulam, Mzee Fortes, Mzee Barmedas- Nera, Nawengine wengi ambao ukiwataja unarudi kabisa nyuma kukumbuka uliko toka..

Alama kama , Uwanja wa Nyamagana, Hospital ya Sekotoure, Clinic, JiweShule ya Lake- Father D'souza, NMwl Magadula, Nyakahoja- Kitovu cha wasomi Mwanza, Nyanza primary, Shule ya Pamba, Shule ya Nyakabungo, Shule ya Makongoro nk.

Ni mhimu kujua Historia ya miji yetu ili vizazi vijavyo, visipoteze kumbu kumbu.





Comments